KAMPUNI YA KAHAMA OIL MILL'KOM' YAJENGA JENGO LA KISASA HOSPITALI YA KAHAMA
Jengo la kisasa la kukaa wananchi wanaofika kusubiri kuona wagonjwa ndugu na jamaa wanaolazwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama ambalo limejengwa kwa msaada wa makampuni ya muwekezaji mzawa ya Kahama Oil Mill kwa gharama ya Sh milioni 11.8 pamoja na kuweka mabenchi ya kukaa watu. Na Patrick Mabula - Kahama Mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Anamringi Macha ameipongeza Kampuni ya Kahama Oil Mill (KOM) inayomilikiwa na mwekezaji mzawa kwa hatua ya kujenga jengo la kisasa la kupumzikia wananchi wanaofika katika hospitali ya wilaya hiyo kuwajulia hali wagonjwa. DC Macha ametoa pongezi hizo jana Jumatatu mjini Kahama wakati akifungua jengo hilo na kueleza kuwa uwepo wa jengo hilo ni msaada kwani utawaondolea adha wananachi kukaa juani na wakati wa masika kunyeshewa na mvua wanapofika kuona wagonjwa ndugu na jamaa zao waliolazwa hospitalini hapo. Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kahama, Lucas David alisema hospitali hiyo ilikuwa inakabiriwa n...